Baadhi ya madenti wa vyuo vikuu mbalimbali jijini Dar es Salaam, wameoza kwa matukio machafu ya ngono.
Katika uchunguzi wa muda mrefu, Inaonyesha kuwa kuna kamtindo ka wanafunzi kufanya mapenzi ndani ya hostel zao huku wakijirekodi na kupiga picha chafu na za aibu na wengine hata kuuza miili yao ili kukidhi hali ngumu ya maisha iliyopo vyuoni
Data zilizokamilika zilionesha kuwa wanafunzi hao waliojulikana kwa jina mojamoja ni Maya mwenye umri wa miaka 19, anayesoma katika chuo maarufu cha mahesabu, Raya anayebukua masomo ya Information Technology (IT) na mwingine ambaye jina lake na chuo anachosoma havikupatikana. Habari zilidai kuwa Raya na rafiki zake watatu wamekuwa wakijihusisha na vitendo haramu vya ngono rejareja na mwanaume mmoja wakiwa katika hosteli hiyo kwa kigezo cha mshiko ‘mnene’ wanaochuma kwa jamaa huyo. Hata hivyo, ripoti ya uchunguzi wetu haikufanikiwa kuwanasa wakimhudumia mwanaume huyo kwa mpigo, isipokuwa ilifuma picha ambazo kila mmoja yuko na jamaa huyo kwa nyakati tofauti.Baada ya kunasa picha hizo chafu kupita maelezo kwa jamii ya Kitanzania, wapekuzi wetu waliwatafuta wahusika ambapo walifanikiwa kumpata Raya ambaye pamoja na kuelezwa kuwa kuna ushahidi wa picha, alikana kuzifahamu. Mbali na matukio hayo yaliyosheheni katika makabrasha yetu, uchunguzi ulibaini kuwa, siyo kila mwanachuo anayepata nafasi hiyo adimu ya kujiunga na elimu ya juu anafanya kile kilichokusudiwa, badala yake wanafanya kinyume kwa kujihusisha na vitendo haramu na hatarishi vya ngono.